Saturday, 20 February 2016

YAJUE HAYA KABLA YA NDOA!!

NI VYEMA UKAYAJUA HAYA KABLA YA KUINGIA KWENYE NDOA:
1. Sherehe ya Harusi ni ya siku moja tu, na Ndoa ni ya maisha yote.

2. Mwanamume/Mwanamke aliyezoea kuchepuka kabla ya Ndoa, ataendelea kuchepuka hata baada ya Ndoa.

3.Upole na ukimya si kiashiria cha tabia njema.

4. Ukikitaka ambacho hakijawahi milikiwa na mtu yeyote, ni lazima ufanye jambo ambalo halijawahi fanywa na mtu yeyote.

5. Mungu akitaka kukubariki hukuletea mtu, na Shetani akitaka kukuangamiza hukuletea mtu. 

6. Bora uishi mwenyewe kuliko kuoa ama kuolewa na mtu asiye sahihi.

7. Aina tatu za wanaume wakuepukwa:
(a) Walevi 
(b) Wazinzi 
(c) Wagomvi.

Aina tano za wanawake wa kuepukwa;
   (a) Walevi
   (b) Wazinzi
   (c) Wachawi
   (d) Wagomvi
   (e) Wasio tii

8 .Kuolewa na Mchekeshaji hakutakufanya uwe na Ndoa yenye furaha.

9. Maneno matatu yanayojenga amani katika Ndoa:
 (a) Nakupenda. 
 (b) Samahani. 
 (c) Asante.

10. Kupiga punyeto kwa mwanaume na kujichua kwa mwanamke ni kuharibu mwili wako mwenyewe.

11. Kuoana kabla ya kuwa marafiki ni kama gari bila mafuta. Hamuwezi kufika popote.

12. Mafanikio ya Ndoa siku zote ni pembetatu:
>Mungu mmoja
> Mume mmoja
> Mke mmoja.

13. Furaha ya kudumu maishani hutegemea na chaguo lako la mwenzi katika Ndoa.

14. Usioe/kuolewa na pesa au mali. Oa/Olewa na mtu. Pesa/Mali hufilisika lakini utu hudumu milele.

15. Uchumba uliovunjika ni bora zaidi kuliko Ndoa isiyo na amani wala furaha.

16. Usiweke kipaumbele chako kwa muonekano mzuri wa mwanamke. Hakuna mwanamke mbaya, bali anahitaji kupendezeshwa.

17. Mapenzi si upofu. Upofu ni kuoa ama kuolewa na mwanamume/mwanamke kwa sababu tu anakidhi haja zako kingono.

18. Ukiwa rafiki mwema, utawavutia marafiki wema. Vivyo hivyo kwa marafiki wabaya (Bad company corrupt good character).

19. Asili ya mikono inayojali ni moyo unaojali.

20. Iepuke Ndoa mbaya kabla haijaanza...

""Mungu awabariki Sana"". 
Watumie na wengine wajifunze.!

Related Posts:

  • WAYS TO KEEP YOUR RELATIONSHIP HAPPYA happy relationship is the goal of anyone who goes into dating. Nobody wants to be in a relationship full of disagreements and fights, and no one most certainly wants to have sleepless nights because they’re seeing somebody … Read More
  • 14 RULES THAT SHOULD GUIDE YOUR RELATIONSHIPNo relationship can succeed without both partners putting in an effort to make it work.Below are 14 rules that should guide your relationship1. “Never push a loyal woman to the point where she no longer cares” – anonymous … Read More
  • 8 WAYS MARRIED COUPLES CAN REMAIN ATTRACTIVE TO EACH OTHERRemaining attracted to each other even after years of being married is no easy feat, but it’s one that shows the marriage is heading in the right direction.One reason many couples falter is because they lose interest in each … Read More
  • 8 QUALITIES OF A RESPECTFUL WOMANA respectful woman is a beautiful woman to have a relationship with or get married to. Though it could be said that some men take advantage of a woman’s respect and treat her with disrespect, but a man who values a good woman… Read More
  • 6 REASONS COUPLES SHOULD DO THINGS TOGETHERIf you notice, couples that do things together stay together; and the opposite is the case when couples don’t do things together.There are so many reasons why couples that do things together would have a healthier, happier re… Read More

1 comment: